Home » » Kazi ya bunge la katiba imeanza, haya ni ya mwanzo tu

Kazi ya bunge la katiba imeanza, haya ni ya mwanzo tu

Written By Unknown on Wednesday, February 19, 2014 | 8:49 AM

Screen Shot 2014-02-19 at 7.37.08 AM
Hatimaye Wajumbe wa Bunge maalum la katiba wameanza vikao vyao February 18 2014 kwa kuelezwa majukumu yao katika kipindi chote watakachoketi kuipitia rasimu ya pili ya katiba mpya ambayo baadae itaunda Katiba mama ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Moja ya jukumu lao kubwa ni kutunza mali za mamlaka ya nchi, kupigavita ubadhirifu, kuhimiza matumizi bora ya rasilimali za nchi huku wakitakiwa kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa na kudumishwa.
Kutokana na hilo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Bunge la Tanzania Kitorina Kippa, amewataka wajumbe wa bunge maalum kutambua kazi wanayoenda kuifanya kuwa haina mshahara na hakutakuwa na malipo baada ya kuhitimisha kazi hiyo.
Mara baada ya ufafanuzi huo, baadhi ya wajumbe akiwemo DK. AVEMARIA SEMAKAFU na JULIUS MTATIRO wamehoji baadhi ya taratibu ikiwemo kuwepo na usawa wa jinsia kwa viongozi watakaoliongoza bunge hilo maalum.
Bunge hili maalum la katiba lilitarajiwa kumchagua Mwenyekiti wa muda atakayeliongoza kwa mpito ili kumpata Mwenyekiti wa kudumu tayari kwa kuunda kanuni zitakazowezesha kujadiliwa kwa rasimu ya pili ya katiba.
Share this article :
 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. Smasher Tz - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger